Maneno ya Griezmann kwa Ribery baada ya kumwambia yeye si world class

11
Bosi wa Atletico Madrid Diego Simeone amesifu ukomavu wa Antoine Griezmann baada ‘kucheka kwa dharau’ kufuatia maneno ya Franck Ribery kwamba yeye sio ‘world class’
Griezmann aliibuka mfungaji bora na kutajwa kuwa mchezaji bora kwenye Michuano ya Euro 2016 baada ya kufunga magoli sita.
Licha ya Griezmann kufanya makubwa yote hayo, winga wa Bayern Munich Frank Ribery ambaye pia ni Mfaransa amesema mchezaji huyo anahitaji muda zaidi ili afikie kuwa world class.
“Kwangu mimi lazima uthibitishe kuwa ni bora kwa kufanya makubwa kwa miaka 10, 12 au 15. Fanya hivyo halafu mimi nitakupongeza,” Ribery alisema.
Griezmann kwa upande wake amejibu kwa kusema: “Mimi nitaendelea kujituma. Kama anavyosema , halafu mwisho wa siku tutaona mimi ni mchezaji wa aina gani, lakini nafahamu fika kwamba niko kwenye mstari sahihi.
“Kila mtu ana maoni yake. Kwa mfano kwa baba yangu, mimi ni mchezaji bora duniani. Vile vile kwa upande wa mashabiki wa timu yangu ya Atletico.”

Share on Google Plus

About omary omary

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment